Idara ya Elimu

You are here:

Utangulizi

Idara hii ni mhimili muhimu katika usimamizi, uratibu, na uendelezaji wa huduma za elimu ndani ya Dayosisi yetu. Idara imejikita katika kutoa elimu bora, jumuishi, na yenye misingi ya kiroho kwa watoto, vijana, na watu wazima, kwa lengo la kuijenga jamii yenye maarifa, maadili na matumaini.

Dayosisi ya Kaskazini Kati ina taasisi za elimu ambazo zimegawanyika katika mkundi makuu matatu.

Shule za msingi

Dayosisi ina shule za msingi (3) zinazoanza na madarasa ya awali hadi darasa la saba. Shule hizi ni shule ya Kimandolu, Ilboru na Tetra (Enkarenarok)

Shule za sekondari

Dayosisi ina shule za sekondari (6) ambazo ni Kimandolu, Ngateu, Enaboishu, Peace House, Moringe na Sekondari ya wasichana wa Maasae.

Vyuo vya Kati

Diyosisi ina chuo cha Teknolojia, Ujasiriamali na Ushirika Monduli (MITEC) na Chuo cha ufundi kilichoko Olokii.

Kila taasisi ina Maono na Utume wake katika kufikia malengo yake ambayo imelenga kwenye Maono na utume wa Dayosisi ya Kaskazini Kati.

Peace House Secondary School

Enaboishu Secondary School