Idara ya Hazina

You are here:

Utangulizi

Idara ya Fedha na Utawala ni nguzo muhimu ya usimamizi wa rasilimali za Dayosisi ya Kaskazini Kati. Lengo kuu la idara hii ni kuhakikisha matumizi ya rasilimali za kifedha, watu, na mali yanazingatia uwajibikaji, uaminifu, ufanisi, na maadili ya Kikristo.

Kwa kushirikiana na vitengo vingine, idara hii inahakikisha kuwa huduma zote za Kiinjili, kijamii na maendeleo zinaendeshwa kwa ufanisi, uwazi, na kwa kuzingatia sheria, taratibu, na kanuni za Kanisa na nchi.

Wajibu wa Idara ya fedha na Utawala

  1. Kuandaa, atasimamia na kutekeleza Sera ya Fedha ya Dayosisi
  2. Kaandaa bajeti Jumuishi ya DKAK na Taasisi zake.
  • Kusimamia utaratibu wa manunuzi kwa mujibu wa sheria za nchi na Kanuni za Manunuzi za Kanisa.
  1. Idara inaandaa hesabu ya mapato na matumizi ya mwaka na kuratibisha ukaguzi wa ndani na nje.
  2. Idara inasimamia teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA).